Connect with us

Fact checking

Mtu anaweza kuambukizwa Virusi vya Corona Baada ya Kupata Chanjo?

Published

on

Ni sababu chache  zinazoweza  kumfanya mtu kupata  virusi vya covid 19 hata baada ya kuchanjwa.

Ripoti zinasema  kuwa chanjo za moderna  na  pfizer  zina asilimia 95 ya uwezo wa kumkinga  mtu, hii ina maana kwamba asilimia 5 ya wanaopewa chanjo  bado wanaweza  kuambukizwa virusi hivi

Uwezekano wa kulazwa hospitalini au kifo kwa aliyepata chanjo ni  wa chini mno ikilinganishwa na ambaye hajachanjwa

Baada ya mtu kupewa chanjo humchukua muda ili  kupata  kinga inayostahili  mwilini  na huchukua wiki mbili zaidi ili awamu ya pili ya dozi ya chanjo aina  ya moderna  kutolewa huku siku 7 kwa dozi ya pili ya pfizer.

Vipimo vya uwezo wa chanjo za covid 19 zinazotolewa na  makampuni ya dawa  hazitoi  picha kamili ya nguvu za chanjo hizo.kutokana na jambo hilo asilimia 5  ya wanaosemekana kuambukizwa virusi hata ingawa wamepokea chanjo yaweza kuwa watu tofauti.

Hakuna chanjo bora zaidi ya nyingine ila kuna sababu zinazochangia kwa chanjo hizi kutofanya kazi ikiwemo  kinga ya chini mwilini

Kuna uwezekano mkubwa kuwa  visa visivyo vya kweli  vya maambukizi  vinavyoripotiwa kuchangia kwa idadi ya wale waliochanjwa  na baadaye  kupatikana na virusi  hivi.

Maafisa wa afya ya umma wanashauri kuvaa barakoa/maski na kuzingatia umbali na mwenzako hata ikiwa umepata chanjo ili wale ambao hawajachanjwa wawe salama na hata virusi visisambae zaidi.

 

 

Editor
+ posts
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *