Connect with us

Habari

Waziri Jumwa Atoa Ahadi kwa Wafanyakazi Serikalini

Published

on

Waziri Aisha Jumwa pamoja na wafanyakazi wa Huduma Center katika siku yake ya kwanza afisini. Picha (Aisha Jumwa; Twitter)

Watumishi wa umma huenda wakapokea nyongeza ya mishahara chini ya miezi mitatu ijayo , amesema waziri wa utumishi wa umma Aisha jumwa.

waziri huyo amesema kamati maalum itaundwa kujadili na kutoa mapendekezo kuhusu mbinu mwafaka itakayotumika kutekeleza nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi hao.

Ni mpango ambao , kulingana na jumwa, unalenga kupunguza visa vya ufisadi serikalini. Amesema ikiwa wafanyakazi wa umma watalipwa vizuri, huenda kusishuhudiwe  visa vya  ufisadi siku za usoni.

Haya yanajiri huku  hazina ya kitaifa ikihangaika kutimiza matakwa ya wafanyakazi wa umma ya nyongeza ya mishahara. Hivi maajuzi, maseneta walitishia kumbandua afisini mkuu wa tume ya kutathmini mishahara ya wafanyikazi wa umma nchini (SRC) lynee Mengich kwa kupunguza mishahara na marupurupu yao.

Tangazo la Jumwa linajiri huku  shirika la fedha ulimwenguni (IMF) likiishinikiza serikali ya rais William Ruto  kupunguza mishahara ya watumishi wa umma  ili  kutenga fedha za kukamilisha miradi ya maendeleo humu nchini.

 

Imehaririwa na Henix Obuchunju 

 

Ken Osoro
+ posts
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *