Connect with us

Habari

watano Hospitalini Baada ya Makabiliano na Polisi

Published

on

 

Watu watano wamelazwa katika hospitali ya Mama Lucy hapa jijini Nairobi baada ya kuumia wakati polisi walikua wakifyatua risasi katika kivuko cha reli cha Total eneo la Dandora. Mkuu wa polisi katika kaunti ndogo ya Kamkunji Francis Kamau alisema polisi walikuwa wakilinda doria wakati walipogundua wizi wa kimabavu uliokuwa ukiendelea. Polisi  walifyatua risasi walipokuwa wakikabiliana na wezi.

Kulingana na ripoti ya  polisi, simu nne zilipatikana katika eneo la mkasa, moja kati ya simu hizo  ilitambuliwa na mwathiriwa wa wizi na kuandikisha taarifa  katika kituo cha polisi cha Dandora. Kati ya wale walioumia wakati wa sarakasi hizo ni abiria waliokuwa wakisubiri kuabiri gari.

Wakaazi wa eneo hilo wameeleza hofu na wasiwasi kuwa huenda polisi waliwapiga risasi wale wasio na hatia. Kamanda wa polisi wa eneo la Dandora  alidai kuwa mshukiwa mmoja alikamatwa na yupo chini ya uangalizi  wa polisi katika hospitali ya Mama Lucy akiendelea kupata matibabu akiwa  anaauguza majeraha ya risasi.

 

Ken Odhiambo
+ posts
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *