Connect with us

Habari

Serikali Yabadilisha Mbinu za Kushawishi Wakenya Kupokea Chanjo

Published

on

(Kushoto ) Waziri wa usalama Fred Matiangi (kati) John Mbadi (Kulia )Waziri wa afya Mutahi Kagwe Picha (Stephen Onyango)

Serikali  imeonekana kubadilisha mfumo wa kuwataka wakenya kupokea chanjo , kutoka kwenye mfumo wa lazima hadi kwenye mfumo wa  kuwashawishi wakenya kupokea chanjo ya COVID -19.

Wakiwa kwenye uzinduzi  wa kuhamasisha wananchi kupokea chanjo  eneo la Dagoreti hapo jana, mawaziri  Fred Matiangi (Usalama wa ndani ) mwenzake wa afya Mutahi kagwe pamoja na Mkurugenzi wa huduma za jiji la nairobi NMS John Mbadi walisisitiza umuhimu wa kila mkenya kupata chanjo ya virusi vya corona  .

Waziri Matiangi alisisitiza kuwa wizara ya usalama itashirikiana pamoja na wizara ya afya kuhakikisha  wakenya wamepata huduma za kupokea chanjo kwa njia ya upole bila mtu yeyote kushurutishwa.“Mpango wa serikali sasa ni kuhakikisha kwamba tumesaidiana sisi wote .” alisema Waziri Matiangi .

Bw Kagwe aliwataka wakenya kuhakikisha wanachukua jukumu la kibinafs kujikinga dhidi ya virusi vya corona . “Jukumu la kukinga maisha yako ni lako ,jukumu la kukinga familia yako ni lako , jukumu la kukinga Watoto wako ni lako ” alisema waziri kagwe alipokuwa akihutubia umma.

Waziri kagwe pia alitupilia mbali dhana ambazo watu wamekuwa nazo kuhusu chanjo  ya virusi vya corona .  “Nasikia hadithi nyingi zikisemwa juu ya hii chanjo, wale wengine wanasema eti  ukidungwa huwezi  kulala , mimi nimedungwa nalala kabisaa.”

Wakaazi wa Nairobi ambao hawajapokea chanjo ya pili walihamasishwa kujitokeza  ili kupata chanjo ya pili “ langu ni kuwasihi wale ambao wamepata chanjo ya kwanza kuhakikisha kuwa wamechanjwa kwa mara ya pili. ”

 

 

 

 

 

Steven Onyango
+ posts
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *