Connect with us

Habari

Mfanyibiashara Afungwa Jela Miaka 23

Published

on

Mfanyabiashara Tom Mboya akiwa mahakamani        ( Picha hisani )

Mfanyabiashara  Tom Mboya amehukumiwa kifungu cha miaka 23 jela kwa kupatikana na  hatia ya kumpiga risasi na kumjeruhi  miliki wa mgahawa wa Ranalo  Foods Bw William Osewe .

Ni  uamuzi uliofanywa na Jaji Martha Mutuko  wa mahakama ya Milimani Jumatano 6/10/ 2021.

 Kwenye mahakama ya Milimani ,“Nimetizama  ripoti iliyowasilishwa  mbele yangu  na kunakili kuwa mshtakiwa , Tom Mboya  hajajutia  kwa lolote lile kutokana na  kitendo alichofanya “ alisema jaji Martha

Mahakama pia ilirejelea dhana kuwa  mshtaki Osewe  aliathirika na bado kufikia sasa ana madhara  ya kupigwa risasi

 “Namhukumu mshtakiwa  kwa miaka 20 jela  kwa kujaribu kutekeleza mauaji na miaka mitatu kwa kujeruhi “ alisema  jaji Mutuku.

 Bw Mboya anadaiwa kumpiga risasi  mara kadha   Bw Osewe Mwezi Disemba mwaka wa 2016  katika eneo la Garden Estate eneo bunge la kasarani  walipokuwa na mzozo kuhusu mwanamke anayefahamika kwa jina  Bi Stella Mutheu

Bw Osewe alilazwa kwenye hospitali ya Aga Khan ambapo alifanyiwa upasuaji kadha ili kuondoa risasi alizokuwa amepigwa .

 Bw Mboya alijisalimisha kwenye kituo cha polisi na kufikishwa mahakamani  alipojitetea dhidi ya mashtaka mwaka wa 2017  na kuachiliwa kwa bondi ya shilingi Ksh 300,000

Stephen Onyango
+ posts
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *