Connect with us

Habari

Kenya Kupokea Chanjo Zingine

Published

on

Kenya inatarajiwa kupokea dozi  milioni 1.7 za Modena na dozi 390,000 za  johnson & johnson  wiki ijayo ya Agosti  23, 2021.

Waziri wa afya mutahi kagwe  akizungumza Jumatano  Agosti 18,2021  amesema kuwa taifa pia linatarajiwa kupokea dozi zingine za Pfeizer  katikati ya mwezi septemba mwakani.

Bw . kagwe pia amehimiza wakenya kupoke chanjo ya virusi vyaa corona kwani ni mojawapo ya kinga inayosaidia kudhibiti virusi vya corona

“Chanjo ni mojawapo ya kinga inayosaidia kukinga  virusi vya corona “amesema waziri kagwe

Hili linakuja bada ya serikali kupokea dozi za  407, 000  za astrazeneka kutoka nchini uingereza na kupokelewa na Mkurugenzi wa afrya Patrick Amoth kwenye uwanja wa ndege wa  Jomo Kenyatta .

 Hii ikiwa ni mojawapo ya mipango ya serikali ya kuchanja watu milioni 26 ifikiapo Juni mwaka ujao na watu milioni 10 kufikia mwezi Disemba mwakani .

Asilimia 2.8 ya wakenya tayari wamepokea chanjo  ya astarzeneca  kwa awamu ya  kwanza na awamu ya pili ,idadi kamili ya watu waliopokea chanjo kiakmiifu ikiwa ni  754,542.

Kufikia sasa wafanyakazi wa afya 127,457  wamepokea chanjo kikamilifu  Mafisa wa usalama 61,974, watu wenye umri wa miaka 58 na zaidi   229,699 , walimu 111,805, na idadi ya watu  223,607 kutoka kwa uma wakiwa wamepokea chanjo kufikia sasa .

Stephen Onyango
+ posts
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *