Connect with us

Habari

BABU OWINO ATANGAZA MSIMAMO

Published

on

The Kenyan Paliamentary Website

 

Mbunge wa Embakasi Mashariki  Paul Ongili, almarufu kama Babu Owino, ameeleza imani yake ya kunyakua kiti cha ugavana  katika kaunti ya Nairobi kwenye uchaguzi mkuu mwaka wa  2027.

Kulingana na Babu Owino, ana kila anachohitaji  kumpiku gavana Johnson Sakaja kwenye uongozi wa kaunti ya Nairobi.

“ Gavana Sakaja anapasha hicho kiti moto, angalia bunge la kitaifa sasa, angalia magavana, angalia maseneta, angalia woman Reps na MCAs….kuna aliye bora kuliko Babu Owino hapo? Sijisifu, niambie tu,” Babu alisema haya  kwenye mahojiano wa matandao wa   YouTube kinachotambuliwa kama ‘Convo Unscripted.  “Naweza kukuambia, 101%. Yeye (Sakaja) nikishika nafasi tu…Sakaja amewekwa hapo ili kunisafishia njia.”

Babu Owino anahudumu  kwa muhula wa  pili  kama mbunge wa Embakasi mashariki  na amezidisha  umaarufu  miongoni mwa vijana.

Kabla ya kujitosa katika siasa za kitaifa babu Owino alihudumu  kwa muda kama mwenye kiti wa muungano wa  wanafunzi  (SONU)  chuo kikuu cha Nairobi.

Charity Kilei
+ posts
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *